Wednesday, 23 October 2013

DOGO JANJA KUTIMULIWA MTANASHATI


Hatimaye Dogo Janja ametimuliwa rasmi Mtanashati Entertainment kwa kile Ostaz Juma alichokidai kwamba Dogo Janja hana nidhamu,kukataa kusoma Shule na kutokuenekana nyumbani mara kwa mara.

Huu ndio ujumbe wa Ostaz Juma Baada ya kuzungumza na mtandao wa Bongo 5 leo Octoba 23 2013

Nimemfukuza Dogo Janja kwasababu hana Heshima,amekimbia Nyumbani,anakoishi sikujui,nimemtafutia Shule amekataa kusoma yaani kwa kifupi simuelewi na mimi ni mzazi ambaye nimekabidhiwa kumlea.Kwa hiyo amenishinda namrudisha kwa wazazi wake

Kwa upande wa Dogo aliulizwa na kusema hivi 'Ostaz ana matatizo yake,naye ni binadamu kama binadamu wengine kwa hiyo mimi nasema amenifukuza ila sio kwasababu ya kuvuta Bangi wala sijakataa Shule.Ningependa tuliache hili Swala mpaka tutakapokutana Kifamilia ndipo tutajua sababu aliyonifukuza ila sio hizo alizozitaja'Alisema Dogo Janja

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...